Hatua muhimu za kujiunga na chama cha wafanyakazi madaktari na wafamasia Tanzania
- Category: Taarifa
- Published: Thursday, 26 October 2023 08:22
- Written by bitta magesa rusweka
- Hits: 266
Hatua ya kwanza
Pakua fomu ya kujiunga TUF 15
Hatua ya pili
jaza fomu kwa mpangilio ufuatao
a.Mstari wa kwanza andika majina yako kamili
b.Mstari wa pili jaza chek namba yako/au nambari ya kitambulisho chako
c.Mstari wa tatu jaza jina la mwajiri wako.jina linaweza kuwa/taasisi/Hospitali unayofanyia kazi/kituo chako cha kazi
Hatua ya tatu ya fomu
weka sahihi yako kwenye mstari unaonekana chini ya fomu (Employee signature) na mbele weka tarehe ya kujiunga
Mstari wa mwisho mpe mtu yoyote kuwa anayekushuhudia ukijaza fomu anaweza kuwa mfanyakazi mwenzako,Rafiki yako au yoyote mwenye umri zaidi ya 18 na akili timamu
Hatua ya nne
Juu ya fomu andika/jaza kodi ya makato ya chama TMDPWU-Deduction code namba PC) 7018)
piga picha fomu yako ya kujiunga na uscan vizuri/aupi picha itume kwa barua pepe zifuatazo
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. au This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. au whassp number 0673420443/0713910324
Hatua ya tano
jaza juu ya fomu yako kodi ya chama (DEDUCTION CODE PC 7018) na wasilisha fomu yako ofisi ya mwajiri wako /utawala/afisa utumishi ili aweke jina lako katika orodha ya makato ya chama.
Muhimu kuzingatia
Vigenzo vya kuwa mwanachama uwe Daktari wa ngazi zote kuanzia cheti hadi huduma bobezi na wafamasia kuanzia ngazi ya cheti hadi huduma bobezi.
Jiunge sasa na chama cha kada yako.
kwa ufafanuzi zaidi tupigie 0713910324/0756477968/0787941606/0673420443.
