DIBAJI
Katiba hii ya kwanza ya TMDPWU ya mwaka 2011 inatokana na maamuzi ya kikao kilichofanyika tarehe26/8/2011 cha madaktari na Wfamasia kupitia mkutano mkuu wa Chama Cha Madaktari na Wafamasia Tanzania na makubaliano kati ya Madaktari na Wafamasia kuunda chama kitakachosimamia maslahi ya wafanyakazi madaktari na wafamasiawote Tanzania.
TMDPWU itamilikiwa nakuendeshwa na wanachama kupitia vyombo vyake na itaimarisha mshikamano na umoja miongoni mwa wanachama wake, na wanachama wengine wa vyamavya wafanyakazi duniani. Aidha TMDPWU itaimarisha na kuendeleza mahusiano mazuri bainayake na Serikali,waajiri,Vyama vya kitaaluma na wadau wote.
TMDPWU itahakikisha kuheshimiwa kwa uhuru wa vyama vya Wafanyakazi, utetezi wa haki namaslahi ya Wafanyakazi, ajira yenye hadhi na masuala yote yanayohusu hifadhi na ustawi wawafanyakazi. Katiba ya TMDPWU ndio zana kuu itakayoongoza utekelezaji wa shughuli za Chama. Katiba yaTMDPWU itaendelea kufanyiwa marekebisho pale wanachama kwa kupitia wawakilishi wao watakapoona inafaa.
Hivyo, wanachama, Viongozi na watendaji wa TMDPWU katika ngazi zote wanapaswa kuiheshimu Katiba hii na kuhakikisha kuwa uongozi na utendaji wa Chama hauendi kinyume namaelekezo yanayotolewa na Katiba hii.